Hatua zinazochukuliwa na
serikali za kukabiliana na kipindu pindu ni nzuri lakini zitafanikiwa endapo
zitatekelezwa na kuendelezwa na wananchi husika katika maeneo yao.
Hayo yamesemwa na wananchi
mbali mbali wakati wakiongea na redio Fadeco katika kipindi cha
HABA NA HABA ambacho
kilikuwa kinahoji hatua zinazochukuliwa na
serikali kukabiliana na ugonjwa
wa kipindu pindu.
Mmoja wa wananchi hao Ponsian
Kanyamuka kutoka Wilayani Kyerwa amesema mikakati ya serikali kuhusu
kukabiliana na ugonjwa wa kipindu pindu zinapaswa kuzingatiwa na wananchi
katika maeneo yao na kuifanya kuwa
endelevu.
Wamesema mpaka sasa hali
usafi katika mazingira ya wananchi ni ya kuridhisha kutokana na kuwa tayari
wamekwisha kupata elimu ya kutosha kutoka kwa viongozi na wamesisitiza kuwa
zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu kwa wananchi wakishirikiana na viongozi wao.
No comments:
Post a Comment